Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 18:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Musa akachagua wanaume wanaostahili miongoni mwa Waisraeli wote na kuwaweka kuwa viongozi wa watu, kuwa wakuu wa maelfu, wakuu wa mamia, wakuu wa hamsini, na wakuu wa makumi.

  • Hesabu 1:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Hao ndio waliochaguliwa miongoni mwa Waisraeli. Hao ndio wakuu+ wa makabila ya baba zao, viongozi wa maelfu katika Israeli.”+

  • Yoshua 22:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kisha Waisraeli wakamtuma Finehasi+ mwana wa kuhani Eleazari kwa watu wa kabila la Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase katika nchi ya Gileadi, 14 na wakuu kumi walikuwa pamoja naye, mkuu mmoja kwa ajili ya kila ukoo* katika makabila yote ya Israeli, kila mmoja wao alikuwa kiongozi wa ukoo wake* miongoni mwa maelfu ya* Israeli.+

  • Yoshua 23:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Yoshua aliwaita Waisraeli wote,+ wazee wao, viongozi wao, waamuzi wao, na wakuu wao,+ akawaambia hivi: “Nimezeeka na umri wangu umesonga sana.

  • 1 Mambo ya Nyakati 27:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Hii ndiyo idadi ya Waisraeli, viongozi wa koo,* wakuu wa maelfu na wa mamia,+ na maofisa wao waliomhudumia mfalme+ katika kila jambo lililohusu vikundi ambavyo viliingia ndani na kutoka nje mwezi baada ya mwezi, miezi yote ya mwaka; kila kikundi kilikuwa na watu 24,000.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki