18 “Waambie hivi Haruni na wanawe na Waisraeli wote: ‘Mwanamume Mwisraeli au mgeni katika Israeli anapomtolea Yehova dhabihu ya kuteketezwa+ ili kutimiza nadhiri zake au kutoa toleo la hiari,+ 19 anapaswa kutoa ng’ombe dume asiye na kasoro,+ wanakondoo dume, au mbuzi ili apate kibali.