-
Mwanzo 38:7-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Lakini Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alimchukiza Yehova; kwa hiyo Yehova akamuua. 8 Kwa hiyo, Yuda akamwambia Onani: “Lala na mke wa ndugu yako na ufunge naye ndoa ya ndugu mkwe, umpe ndugu yako mzao.”+ 9 Lakini Onani alijua kwamba mzao huyo hangehesabiwa kuwa wake.+ Kwa hiyo alipolala na mke wa ndugu yake, alimwaga shahawa zake ardhini ili asimpe ndugu yake mzao.+ 10 Jambo alilofanya lilikuwa ovu machoni pa Yehova, kwa hiyo akamuua pia.+
-