- 
	                        
            
            Yoshua 13:24-28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
24 Pia, Musa akawapa urithi watu wa kabila la Gadi, kulingana na koo zao, 25 na eneo lao lilitia ndani Yazeri+ na majiji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Waamoni+ hadi Aroeri, mbele ya Raba;+ 26 na kutoka Heshboni+ hadi Ramath-mispe na Betonimu, na kutoka Mahanaimu+ hadi mpaka wa Debiri; 27 na bondeni,* Beth-haramu, Beth-nimra,+ Sukothi,+ na Safoni, eneo lililobaki la Mfalme Sihoni wa Heshboni,+ na Mto Yordani ulikuwa mpaka ulioanzia upande wa chini wa Bahari ya Kinerethi,*+ upande wa mashariki wa Yordani. 28 Huo ndio uliokuwa urithi wa kabila la Gadi kulingana na koo zao, pamoja na miji na vijiji vyake.
 
 -