-
Hesabu 32:1-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
32 Sasa wana wa Rubeni+ na wana wa Gadi+ walikuwa na mifugo mingi sana, wakaona kwamba eneo la Yazeri+ na eneo la Gileadi yalikuwa maeneo mazuri kwa mifugo. 2 Basi wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakaja kwa Musa, kuhani Eleazari, na wakuu wa Waisraeli na kuwaambia hivi: 3 “Atarothi, Diboni, Yazeri, Nimra, Heshboni,+ Eleale, Sebamu, Nebo,+ na Beoni,+ 4 maeneo ambayo Yehova aliyashinda mbele ya Waisraeli,+ ni maeneo mazuri kwa mifugo, nasi watumishi wenu tuna mifugo mingi.”+ 5 Wakaendelea kusema, “Ikiwa sisi watumishi wenu tumepata kibali machoni penu, tupeni maeneo haya tuyamiliki. Msituvushe ng’ambo ya Mto Yordani.”
-