6 “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ni Yehova, nami nitawatoa kutoka chini ya mizigo ya Wamisri na kuwaokoa kutoka katika utumwa wao,+ nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa* na kwa hukumu kubwa.+
3 Ndipo Musa akawaambia watu: “Kumbukeni siku hii mliyotoka Misri,+ kutoka katika nyumba ya utumwa, kwa sababu kwa mkono wenye nguvu Yehova aliwatoa katika nchi hii.+ Kwa hiyo hampaswi kula kitu chochote kilichotiwa chachu.
14 “Mwanao akikuuliza baadaye, ‘Jambo hili linamaanisha nini?’ basi unapaswa kumwambia, ‘Kwa mkono wenye nguvu Yehova alitutoa Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa.+