Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 26:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 nitawaletea mvua katika majira yanayofaa,+ nayo nchi itazaa kwa wingi,+ na miti ya matunda itazaa matunda mengi.

  • Kumbukumbu la Torati 8:7-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwa maana Yehova Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri,+ nchi yenye vijito vya maji, mabubujiko na chemchemi zinazotiririka* katika bonde tambarare na katika eneo lenye milima, 8 nchi yenye ngano na shayiri, na mizabibu, mitini, na mikomamanga,+ nchi yenye mafuta ya zeituni na asali,+ 9 nchi ambayo haitakuwa na upungufu wa chakula na hamtakosa chochote, nchi yenye mawe yaliyo na chuma na katika milima yake mtachimba shaba.

  • Kumbukumbu la Torati 28:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Yehova atawafungulia ghala lake zuri, mbingu, ili mvua inyeshe juu ya nchi yenu katika majira yake+ na kubariki kila jambo mnalofanya. Mtayakopesha mataifa mengi, lakini ninyi wenyewe hamtahitaji kukopa.+

  • Yeremia 14:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Je, kuna sanamu yoyote kati ya sanamu za ubatili za mataifa inayoweza kuleta mvua,

      Au, je, hata mbingu zinaweza kuleta mvua zenyewe?

      Je, si Wewe peke yako, Ee Yehova Mungu wetu?+

      Nasi tunakutumaini,

      Kwa maana wewe peke yako ndiye uliyefanya mambo hayo yote.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki