11 Mtaleta vitu vyote ninavyowaamuru mahali ambapo Yehova Mungu wenu atachagua jina lake likae hapo+—dhabihu zenu za kuteketezwa, matoleo yenu, sehemu zenu za kumi,+ mchango kutoka mkononi mwenu, na kila dhabihu ya nadhiri mnayoweka nadhiri kwa Yehova.
12 “Baada ya kutoa sehemu yote ya kumi+ ya mazao yako katika mwaka wa tatu, mwaka wa sehemu ya kumi, utampa sehemu hiyo Mlawi, mkaaji mgeni, yatima, na mjane, nao watakula na kushiba katika majiji*+ yenu.