-
Kumbukumbu la Torati 29:10-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 “Leo ninyi nyote mmesimama mbele za Yehova Mungu wenu; viongozi wa makabila yenu, wazee wenu, maofisa wenu, kila mwanamume wa Israeli, 11 watoto wenu, wake zenu,+ na mkaaji mgeni+ anayeishi kambini mwenu, kuanzia mtu anayewakusanyia kuni mpaka anayewatekea maji. 12 Mko hapa ili mwingie katika agano la Yehova Mungu wenu na kiapo chake, agano ambalo Yehova Mungu wenu anafanya pamoja nanyi leo+ 13 ili leo awafanye ninyi kuwa watu wake+ na ili awe Mungu wenu,+ kama alivyowaahidi ninyi na kama alivyowaapia mababu zenu, Abrahamu,+ Isaka,+ na Yakobo.+
-