Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 1:39, 40
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 Kisha Kuhani Sadoki akachukua pembe ya mafuta+ kutoka hemani+ na kumtia mafuta Sulemani,+ nao wakaanza kupiga pembe, na watu wote wakaanza kusema hivi kwa sauti kubwa: “Mfalme Sulemani na aishi muda mrefu!” 40 Kisha watu wote wakapanda wakimfuata, wakipiga filimbi na kushangilia sana, hivi kwamba dunia ikapasuka na kufunguka kwa sababu ya kelele zao.+

  • 2 Wafalme 11:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kisha Yehoyada akamtoa nje mwana wa mfalme+ na kumvika taji na Ushahidi,*+ wakamweka kuwa mfalme na kumtia mafuta. Wakaanza kupiga makofi na kusema: “Mfalme na aishi muda mrefu!”+

  • 2 Wafalme 11:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kisha akamwona mfalme akiwa amesimama hapo kando ya nguzo kama ilivyokuwa desturi.+ Wakuu na wapiga tarumbeta+ walikuwa pamoja na mfalme, na watu wote nchini walikuwa wakishangilia na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akayararua mavazi yake na kupaza sauti: “Ni njama! Ni njama!”

  • 1 Mambo ya Nyakati 12:39, 40
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 Nao walikaa huko pamoja na Daudi kwa siku tatu, wakila na kunywa, kwa kuwa ndugu zao walikuwa wamefanya matayarisho kwa ajili yao. 40 Pia majirani wao, na hata wale waliokuwa mbali kufikia Isakari, Zabuloni, na Naftali, walikuwa wakileta vyakula kwa punda, ngamia, nyumbu, na ng’ombe—walileta unga, keki za tini zilizoshinikizwa na keki za zabibu kavu, divai, mafuta, na ng’ombe na kondoo wengi sana, kwa maana watu walishangilia nchini Israeli.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki