20 Kisha nabii Miriamu, dada ya Haruni, akachukua tari, na wanawake wote wakamfuata wakiwa na matari yao wakicheza dansi. 21 Miriamu akaimba hivi akiwaitikia wanaume:
“Mwimbieni Yehova, kwa maana amekwezwa sana.+
Farasi na mpandaji wake amewavurumisha baharini.”+