-
1 Mambo ya Nyakati 11:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Baada ya muda Waisraeli wote wakakusanyika kwa Daudi kule Hebroni+ na kusema: “Tazama! Sisi ni mfupa wako na nyama yako.*+ 2 Zamani, Sauli alipokuwa mfalme, ni wewe uliyewaongoza Waisraeli vitani.*+ Na Yehova Mungu wako alikuambia hivi: ‘Utawachunga watu wangu Waisraeli, nawe utakuwa kiongozi wa watu wangu Waisraeli.’”+ 3 Basi wazee wote wa Israeli wakaja kwa mfalme huko Hebroni, na Daudi akafanya agano nao huko Hebroni mbele za Yehova. Kisha wakamtia mafuta Daudi awe mfalme wa Israeli,+ kulingana na neno la Yehova kupitia Samweli.+
-