18 Basi Abigaili+ akachukua haraka mikate 200, mitungi miwili mikubwa ya divai, kondoo watano waliochinjwa, sea tano* za nafaka iliyokaangwa, keki 100 za zabibu kavu, na keki 200 za tini zilizoshinikizwa, akapakia vitu hivyo vyote juu ya punda.+
2 Mfalme akamuuliza Siba: “Kwa nini umeleta vitu hivi?” Siba akamjibu: “Punda ni kwa ajili ya nyumba ya mfalme ili wapande juu yao, mikate na matunda ya kiangazi ni kwa ajili ya vijana, na divai ni kwa ajili ya wale watakaochoka nyikani.”+