-
Ezekieli 41:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Vyumba vya kando vilikuwa na ghorofa tatu, moja juu ya nyingine, na kila ghorofa ilikuwa na vyumba 30. Kulikuwa na vidato kuzunguka pande zote za ukuta wa hekalu ambavyo vilishikilia vyumba vya kando, ili vishikio visiguse ukuta wa hekalu lenyewe.+ 7 Pande zote mbili za hekalu zilikuwa na njia iliyopindapinda* ambayo ilipanuka kadiri ilivyopanda kuelekea vyumba vya juu.+ Upana uliongezeka kutoka ghorofa moja hadi nyingine kadiri mtu alivyopanda kutoka ghorofa ya chini hadi ya juu akipitia ghorofa ya katikati.
-