-
2 Mambo ya Nyakati 5:11-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Makuhani walipotoka mahali patakatifu (kwa maana makuhani wote waliokuwepo walikuwa wamejitakasa,+ bila kuzingatia vikundi vyao),+ 12 waimbaji wote Walawi+ walioongozwa na Asafu,+ Hemani,+ Yeduthuni,+ wana wao na ndugu zao walikuwa wamevaa mavazi ya kitambaa bora, wakiwa wamebeba matoazi, vinanda, na vinubi; walikuwa wamesimama upande wa mashariki wa madhabahu, na makuhani 120 waliokuwa wakipiga tarumbeta walikuwa pamoja nao.+ 13 Mara tu wapiga tarumbeta na waimbaji walipoanza kumsifu na kumshukuru Yehova kwa pamoja, na milio ya tarumbeta, matoazi, na ala nyingine za muziki zilipoanza kusikika walipokuwa wakimsifu Yehova, “kwa maana yeye ni mwema; upendo wake mshikamanifu unadumu milele,”+ ndipo nyumba hiyo, nyumba ya Yehova, ikajaa wingu.+ 14 Makuhani hawakuweza kusimama ili kuhudumu kwa sababu ya wingu hilo, kwa maana utukufu wa Yehova ulijaa katika nyumba ya Mungu wa kweli.+
-