-
2 Mambo ya Nyakati 6:14-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 akasema: “Ee Yehova Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe mbinguni wala duniani, unayeshika agano na kuwatendea kwa upendo mshikamanifu watumishi wako wanaotembea mbele zako kwa moyo wao wote.+ 15 Umetimiza ahadi uliyomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu.+ Ulitoa ahadi hiyo kwa kinywa chako mwenyewe, na siku ya leo umeitimiza kwa mkono wako mwenyewe.+ 16 Na sasa, Ee Yehova Mungu wa Israeli, timiza ahadi uliyomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu ulipomwambia, ‘Hutakosa kamwe mwanamume wa uzao wako atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli mbele zangu, ikiwa tu wana wako watakazia uangalifu njia yao kwa kutembea katika sheria yangu,+ kama ulivyotembea mbele zangu.’+ 17 Na sasa, Ee Yehova Mungu wa Israeli, acha ahadi uliyomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu ithibitike kuwa ya kweli.
-