Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 11:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Kisha akamwambia Yeroboamu:

      “Jichukulie vipande kumi, kwa maana Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Tazama, ninaurarua ufalme kutoka mikononi mwa Sulemani, nami nitakupa makabila kumi.+

  • 1 Wafalme 12:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Pia, Yeroboamu akaanzisha sherehe katika mwezi wa nane, siku ya 15 ya mwezi huo, kama ile sherehe iliyokuwa ikifanywa kule Yuda.+ Kwenye madhabahu aliyojenga kule Betheli,+ alitoa dhabihu kwa wale ndama aliokuwa ametengeneza, na huko Betheli akaweka makuhani wahudumu mahali pa juu alipokuwa amejenga.

  • 1 Wafalme 14:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa sababu hiyo ninailetea msiba nyumba ya Yeroboamu, nami nitamwangamiza kila mwanamume* wa Yeroboamu, kutia ndani wasio na uwezo na walio dhaifu katika Israeli, nami nitaifagia kabisa nyumba ya Yeroboamu,+ kama mtu anavyoondoa kabisa mavi mpaka yote yanapokwisha!

  • 2 Mambo ya Nyakati 11:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Walawi waliacha malisho yao na miliki yao+ wakaja Yuda na Yerusalemu, kwa sababu Yeroboamu na wanawe walikuwa wamewaondoa ili wasiwe makuhani wa Yehova.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 13:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Basi Abiya akaenda vitani akiwa na jeshi lenye mashujaa hodari 400,000 waliozoezwa.*+ Na Yeroboamu akajipanga kivita ili kupigana naye akiwa na wanaume 800,000, mashujaa hodari waliozoezwa.*

  • 2 Mambo ya Nyakati 13:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Na Yeroboamu hakupata tena mamlaka* katika siku za Abiya; kisha Yehova akampiga, naye akafa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki