-
1 Samweli 8:11-18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Akasema: “Mfalme atakayewatawala atakuwa na haki ya kudai mambo haya:+ Atawachukua wana wenu+ na kuwafanya wawe waendeshaji wa magari yake ya farasi+ na wapanda farasi wake,+ na baadhi yao watalazimika kukimbia mbele ya magari yake. 12 Naye atajichagulia wakuu wa maelfu+ na wakuu wa hamsini,+ na baadhi yao watamlimia mashamba yake,+ watavuna mazao yake,+ na kutengeneza silaha zake za vita na vifaa vya magari yake.+ 13 Atachukua mabinti wenu na kuwafanya kuwa watengenezaji wa marashi,* wapishi, na waokaji.+ 14 Atachukua mashamba yenu bora, mashamba yenu bora ya mizabibu, na mashamba yenu bora ya mizeituni+ na kuwapa watumishi wake. 15 Atachukua sehemu ya kumi ya mashamba yenu ya nafaka na mashamba yenu ya mizabibu na kuwapa maofisa wa makao yake na watumishi wake. 16 Naye atachukua watumishi wenu wa kiume na wa kike, ng’ombe wenu walio bora, na punda wenu na kuwatumia kufanya kazi zake.+ 17 Atachukua sehemu ya kumi ya kondoo wenu na mbuzi wenu,+ nanyi mtakuwa watumishi wake. 18 Siku itafika mtakapolia kwa sababu ya mfalme ambaye mlijichagulia wenyewe,+ lakini Yehova hatawajibu siku hiyo.”
-