-
2 Wafalme 17:21-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Aliwararua Waisraeli kutoka katika nyumba ya Daudi, nao wakamweka Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme.+ Lakini Yeroboamu akasababisha Waisraeli wapotoke na kuacha kumfuata Yehova, naye akasababisha watende dhambi kubwa. 22 Na Waisraeli wakaendelea kufuata dhambi zote ambazo Yeroboamu alitenda.+ Hawakuziacha 23 mpaka Yehova alipowaondoa Waisraeli kutoka mbele zake, kama alivyokuwa amesema kupitia watumishi wake wote manabii.+ Kwa hiyo Waisraeli wakaondolewa katika nchi yao na kupelekwa uhamishoni kule Ashuru,+ nao wangali huko hadi leo.
-