-
2 Wafalme 23:16, 17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Yosia alipogeuka na kuona makaburi yaliyokuwa mlimani, aliagiza mifupa itolewe katika makaburi hayo na kuteketezwa kwenye madhabahu, akaifanya madhabahu hiyo isifae kwa ibada, kulingana na neno la Yehova lililokuwa limesemwa na mtu wa Mungu wa kweli aliyetabiri kwamba mambo hayo yangetukia.+ 17 Kisha akauliza: “Lile jiwe la kaburi ninaloona pale ni la nani?” Ndipo watu wa jiji hilo wakamjibu: “Ni kaburi la mtu wa Mungu wa kweli kutoka Yuda+ aliyetabiri mambo haya uliyoitendea madhabahu ya Betheli.”
-