31 Na kana kwamba lilikuwa jambo dogo kwake kutembea katika dhambi za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, hata alimwoa Yezebeli+ binti ya Ethbaali, mfalme wa Wasidoni,+ akaanza kumwabudu Baali+ na kumwinamia.
4 na Yezebeli+ alipokuwa akiwaua manabii wa Yehova, Obadia aliwachukua manabii 100 na kuwaficha katika mapango mawili, manabii 50 katika kila pango, naye alikuwa akiwapa mikate na maji.)
2 Ndipo Yezebeli akamtuma mjumbe kwa Eliya, akisema: “Miungu na iniadhibu, tena vikali, ikiwa kufikia kesho wakati kama huu sitakufanya uwe kama* kila mmoja wa manabii hao!”
7 Yezebeli mke wake akamwambia: “Je, si wewe unayetawala ukiwa mfalme wa Israeli? Inuka, kula chakula, moyo wako na uchangamke. Nitakupa shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli.”+