-
2 Wafalme 16:2, 3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Ahazi alikuwa na umri wa miaka 20 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 16 huko Yerusalemu. Hakutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova Mungu wake, kama alivyotenda Daudi babu yake.+ 3 Badala yake, alitembea katika njia ya wafalme wa Israeli,+ na hata alimteketeza* motoni mwana wake mwenyewe,+ akifuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli.
-
-
Yeremia 32:35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
35 Isitoshe, walijenga mahali pa juu pa Baali katika Bonde la Mwana wa Hinomu,*+ ili kuwateketeza* motoni wana wao na mabinti wao kwa ajili ya Moleki,+ jambo ambalo sikuwaamuru,+ na ambalo halijawahi kamwe kuingia moyoni mwangu,* kufanya jambo kama hilo linalochukiza, na kusababisha watu wa Yuda watende dhambi.’
-