-
2 Mambo ya Nyakati 2:4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Sasa ninajenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu, ili niitakase kwake, nifukize uvumba wenye manukato+ mbele zake, na pia kwa ajili ya mikate ya tabaka* inayotolewa daima+ na pia dhabihu za kuteketezwa, asubuhi na jioni,+ nyakati za Sabato,+ miezi mipya,+ na kwenye majira ya sherehe+ za Yehova Mungu wetu. Huu ni wajibu wa kudumu kwa Waisraeli.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 13:11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Wanamfukizia Yehova moshi wa dhabihu za kuteketezwa kila asubuhi na kila jioni+ pamoja na uvumba uliotiwa manukato,+ na mikate ya tabaka*+ iko kwenye meza iliyotengenezwa kwa dhahabu safi, nao wanawasha kinara cha taa cha dhahabu+ na taa zake kila jioni,+ kwa sababu tunatekeleza jukumu letu kwa Yehova Mungu wetu; lakini ninyi mmemwacha.
-