-
2 Mambo ya Nyakati 5:12, 13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 waimbaji wote Walawi+ walioongozwa na Asafu,+ Hemani,+ Yeduthuni,+ wana wao na ndugu zao walikuwa wamevaa mavazi ya kitambaa bora, wakiwa wamebeba matoazi, vinanda, na vinubi; walikuwa wamesimama upande wa mashariki wa madhabahu, na makuhani 120 waliokuwa wakipiga tarumbeta walikuwa pamoja nao.+ 13 Mara tu wapiga tarumbeta na waimbaji walipoanza kumsifu na kumshukuru Yehova kwa pamoja, na milio ya tarumbeta, matoazi, na ala nyingine za muziki zilipoanza kusikika walipokuwa wakimsifu Yehova, “kwa maana yeye ni mwema; upendo wake mshikamanifu unadumu milele,”+ ndipo nyumba hiyo, nyumba ya Yehova, ikajaa wingu.+
-