-
Mwanzo 49:22-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 “Yosefu+ ni chipukizi la mti unaozaa matunda mengi, mti ulio kando ya chemchemi unaozaa matunda mengi, wenye matawi yanayoenea juu ya ukuta. 23 Lakini wapiga mishale waliendelea kumshambulia na kumpiga kwa mishale na kuendelea kuwa na uadui dhidi yake.+ 24 Lakini bado upinde wake ulibaki mahali pake,+ na mikono yake ikaendelea kuwa na nguvu na myepesi.+ Alitiwa nguvu na mikono ya mwenye nguvu wa Yakobo, mchungaji, jiwe la Israeli. 25 Anatoka* kwa Mungu wa baba yako, naye atakusaidia, naye yuko pamoja na Mweza-Yote, atakubariki kwa baraka za mbingu zilizo juu, kwa baraka za vilindi vilivyo chini,+ kwa baraka za matiti na tumbo la uzazi. 26 Baraka za baba yako zitakuwa bora kuliko baraka za milima ya milele, bora kuliko vitu vyenye kutamanika vya vilima vinavyodumu.+ Zitaendelea kuwa juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya utosi wa kichwa cha yule aliyechaguliwa kutoka kati ya ndugu zake.+
-