12 Isitoshe, Absalomu alipotoa dhabihu, aliwatuma watu wamwite Ahithofeli+ Mgiloni, mshauri wa Daudi,+ kutoka jiji la Gilo.+ Njama iliendelea kupamba moto, na idadi ya watu waliomuunga mkono Absalomu ikaendelea kuongezeka.+
23 Siku hizo, ushauri uliotolewa na Ahithofeli+ ulionwa kama neno la* Mungu wa kweli. Hivyo ndivyo ushauri wote wa Ahithofeli ulivyothaminiwa, na Daudi na pia Absalomu.
23 Ahithofeli alipoona kwamba ushauri wake haukufuatwa, aliweka matandiko juu ya punda wake na kwenda nyumbani kwake katika mji wao.+ Baada ya kuwapa maagizo watu wa nyumbani mwake,+ akajitia kitanzi.*+ Basi akafa na kuzikwa katika makaburi ya mababu zake.