36 Yehoyakimu+ alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 11 huko Yerusalemu.+ Mama yake aliitwa Zebida binti ya Pedaya kutoka Ruma. 37 Yehoyakimu aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova,+ alitenda mambo yote ambayo mababu zake walitenda.+