7 Pia, Mfalme Koreshi akaleta vyombo vya nyumba ya Yehova ambavyo Nebukadneza alikuwa amechukua huko Yerusalemu na kuviweka katika nyumba ya mungu wake.+
16 Nami nikawaambia makuhani na watu hawa wote, “Yehova anasema hivi: ‘Msiyasikilize maneno ya manabii wenu wanaowatabiria wakisema: “Tazameni! Vyombo vya nyumba ya Yehova vitarudishwa kutoka Babiloni hivi karibuni!”+ kwa maana wanawatabiria uwongo.+
2 Baada ya muda Yehova akamtia Mfalme Yehoyakimu wa Yuda mikononi mwake,+ pamoja na baadhi ya vyombo vya nyumba ya* Mungu wa kweli, akavileta katika nchi ya Shinari*+ katika nyumba ya* mungu wake. Akaviweka katika hazina ya mungu wake.+
2 Alipokuwa amelewa, Belshaza akaagiza vyombo vya dhahabu na vya fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka katika hekalu la Yerusalemu viletwe,+ ili avitumie kunywea divai pamoja na wakuu wake, masuria wake, na wake zake wadogo.