-
1 Wafalme 12:8-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Hata hivyo, alikataa ushauri aliopewa na wanaume wazee, akashauriana na vijana wa rika lake na ambao sasa walikuwa watumishi wake.+ 9 Aliwauliza: “Mnashauri tuwape jibu gani watu hawa ambao wameniambia, ‘Ifanye nira ambayo baba yako alitutwika iwe nyepesi zaidi’?” 10 Vijana hao wa rika lake wakamwambia: “Hivi ndivyo unavyopaswa kuwaambia watu hao waliokwambia, ‘Baba yako aliifanya nira yetu kuwa nzito, lakini wewe unapaswa kuifanya kuwa nyepesi zaidi kwa ajili yetu’; hivi ndivyo unavyopaswa kuwaambia, ‘Kidole changu kidogo kitakuwa kinene kuliko kiuno cha baba yangu. 11 Baba yangu aliwatwika nira nzito, lakini mimi nitazidisha uzito wa nira yenu. Baba yangu aliwaadhibu kwa mijeledi, lakini mimi nitawaadhibu kwa mijeledi yenye miiba.’”
-