-
2 Wafalme 11:13-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Athalia aliposikia sauti ya watu wakikimbia, mara moja akaja na kujiunga na watu katika nyumba ya Yehova.+ 14 Kisha akamwona mfalme akiwa amesimama hapo kando ya nguzo kama ilivyokuwa desturi.+ Wakuu na wapiga tarumbeta+ walikuwa pamoja na mfalme, na watu wote nchini walikuwa wakishangilia na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akayararua mavazi yake na kupaza sauti: “Ni njama! Ni njama!” 15 Lakini kuhani Yehoyada akawaamuru hivi wakuu wa mamia,+ wale waliowekwa kulisimamia jeshi: “Mwondoeni miongoni mwa vikosi, na yeyote akimfuata, muueni kwa upanga!” Kwa maana kuhani alikuwa amesema: “Msimuue ndani ya nyumba ya Yehova.” 16 Basi wakamkamata, na alipofika mahali ambapo farasi huingia katika nyumba ya* mfalme,+ akauawa hapo.
-