-
2 Wafalme 22:3-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Katika mwaka wa 18 wa Mfalme Yosia, mfalme huyo alimtuma mwandishi Shafani, mwana wa Azalia mwana wa Meshulamu, kwenye nyumba ya Yehova,+ akisema: 4 “Panda uende kwa kuhani mkuu Hilkia+ umwambie akusanye pesa zote zinazoletwa katika nyumba ya Yehova+ ambazo walinzi wa malango wanakusanya kutoka kwa watu.+ 5 Waagize wawape wale waliowekwa kusimamia kazi katika nyumba ya Yehova, ili nao wawape wafanyakazi walio katika nyumba ya Yehova wanaopaswa kurekebisha sehemu zilizoharibika za* nyumba hiyo,+
-