-
2 Wafalme 12:4, 5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Yehoashi akawaambia makuhani: “Chukueni pesa zote zinazoletwa katika nyumba ya Yehova kwa ajili ya matoleo matakatifu,+ pesa ambazo kila mtu amekadiriwa kutoa,+ pesa zilizotolewa kama thamani iliyokadiriwa ya mtu,* na pesa zote ambazo moyo wa kila mtu umemchochea kuleta katika nyumba ya Yehova.+ 5 Makuhani wenyewe watachukua pesa hizo kutoka kwa wale wanaozitoa* na kuzitumia kurekebisha nyumba hiyo, sehemu yoyote iliyoharibika.”*+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 34:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Walienda kwa kuhani mkuu Hilkia na kumpa pesa zilizokuwa zimeletwa katika nyumba ya Mungu, ambazo Walawi waliokuwa walinzi wa malango walikuwa wamekusanya kutoka kwa watu wa kabila la Manase, Efraimu, na Waisraeli wengine wote,+ na pia kutoka kwa watu wa Yuda, Benjamini, na wakaaji wa Yerusalemu. 10 Kisha wakawapa pesa hizo wale waliowekwa kusimamia kazi katika nyumba ya Yehova. Halafu wafanyakazi waliokuwa katika nyumba ya Yehova wakazitumia kuikarabati na kuirekebisha nyumba hiyo.
-