-
2 Wafalme 14:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Kisha Amazia akawatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli, akisema: “Njoo, tupambane vitani.”*+ 9 Mfalme Yehoashi wa Israeli akatuma ujumbe huu kwa Mfalme Amazia wa Yuda: “Gugu lenye miiba kule Lebanoni lilituma ujumbe huu kwa mwerezi huko Lebanoni, ‘Mpe mwanangu binti yako awe mke wake.’ Hata hivyo, mnyama wa mwituni wa Lebanoni akapita karibu na kulikanyaga-kanyaga gugu hilo lenye miiba. 10 Ni kweli kwamba uliwaangamiza Waedomu,+ kwa hiyo moyo wako umekuwa na kiburi. Furahia utukufu wako, lakini kaa katika nyumba yako mwenyewe.* Kwa nini utafute msiba kisha uanguke, na kuwaangusha pia watu wa Yuda?”
-