-
2 Wafalme 14:17-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Amazia+ mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda aliendelea kuishi kwa miaka 15 baada ya kifo cha Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.+ 18 Na mambo mengine katika historia ya Amazia, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 19 Baadaye njama ikapangwa dhidi yake+ huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatie huko Lakishi, nao wakamuua huko. 20 Kwa hiyo wakambeba juu ya farasi, naye akazikwa Yerusalemu pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+
-