-
2 Wafalme 9:17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Mlinzi aliyekuwa amesimama juu ya mnara huko Yezreeli aliona kundi kubwa la wanaume wa Yehu likija. Mara moja akasema: “Ninaona kundi kubwa la wanaume.” Yehoramu akasema: “Chukua mpanda farasi mmoja umtume akutane nao, awaulize, ‘Je, mmekuja kwa amani?’”
-
-
2 Mambo ya Nyakati 26:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Isitoshe, Uzia alijenga minara+ Yerusalemu karibu na Lango la Pembeni,+ Lango la Bondeni,+ na Nguzo ya Kutegemeza Ukuta, naye akaiimarisha. 10 Pia, alijenga minara+ nyikani na kuchimba* matangi mengi ya maji (kwa maana alikuwa na mifugo mingi sana); alifanya hivyo pia katika Shefela na katika nchi tambarare ya juu. Alikuwa na wakulima na watunzaji wa mizabibu milimani na kule Karmeli, kwa maana alipenda kilimo.
-