-
2 Mambo ya Nyakati 15:10-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Basi wakakusanywa pamoja Yerusalemu katika mwezi wa tatu wa mwaka wa 15 wa utawala wa Asa. 11 Siku hiyo walimtolea Yehova dhabihu kutoka katika nyara walizoleta, ng’ombe 700 na kondoo 7,000. 12 Zaidi ya hayo, walifanya agano ili kumtafuta Yehova Mungu wa mababu zao kwa moyo wao wote na kwa nafsi* yao yote.+ 13 Mtu yeyote ambaye hangemtafuta Yehova Mungu wa Israeli angeuawa, awe mdogo au mkubwa, awe mwanamume au mwanamke.+
-