-
Mambo ya Walawi 4:13, 14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 “‘Sasa ikiwa kusanyiko lote la Waisraeli lina hatia ya kutenda dhambi bila kukusudia,+ lakini halikujua kwamba limefanya jambo ambalo Yehova aliamuru lisifanywe,+ 14 kisha dhambi hiyo ijulikane, ni lazima kusanyiko litoe ng’ombe dume mchanga kwa ajili ya dhabihu ya dhambi na kumleta mbele ya hema la mkutano.
-
-
Hesabu 15:22-24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 “‘Sasa mkifanya kosa, nanyi mkose kushika amri hizi zote ambazo mimi, Yehova, nimempa Musa, 23 mambo yote ambayo mimi, Yehova, nimewaamuru ninyi kupitia Musa katika vizazi vyenu tangu siku ambayo mimi Yehova niliamuru, 24 na ikiwa kosa hilo lilifanywa bila kukusudia na bila kusanyiko lote kujua, basi ni lazima kusanyiko lote litoe dhabihu ya kuteketezwa ya ng’ombe dume mchanga ili iwe harufu inayompendeza* Yehova, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji kulingana na utaratibu wa kawaida,+ na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi.+
-