-
1 Mambo ya Nyakati 23:27-30Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
27 Kwa maana kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi wenye umri wa miaka 20 na zaidi walihesabiwa. 28 Jukumu lao lilikuwa kuwasaidia wana wa Haruni+ katika utumishi wa nyumba ya Yehova, kusimamia nyua,+ vyumba vya kulia chakula, kukitakasa kila kitu kitakatifu, na kazi yoyote iliyohitaji kufanywa katika utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli. 29 Waliwasaidia katika kazi ya mikate ya tabaka,*+ unga laini wa toleo la nafaka, mikate myembamba isiyo na chachu,+ keki zilizookwa, unga wa kukandwa uliochanganywa,+ na vipimo vyote vya wingi na ukubwa. 30 Walipaswa kusimama asubuhi baada ya asubuhi+ ili kumshukuru na kumsifu Yehova, na walipaswa kufanya hivyo jioni pia.+
-