-
Mambo ya Walawi 5:17, 18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 “Mtu akitenda dhambi kwa kufanya jambo lolote ambalo Yehova ameamuru lisifanywe, hata kama hajui, bado ana hatia naye atawajibika kwa sababu ya kosa lake.+ 18 Anapaswa kumletea kuhani kondoo dume asiye na kasoro kutoka kundini kulingana na thamani iliyokadiriwa, kwa ajili ya dhabihu ya hatia.+ Kisha kuhani atamtolea dhabihu ya kufunika kosa alilofanya bila kukusudia na bila kujua, naye atasamehewa.
-