-
Ezra 4:14, 15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Na kwa kuwa sisi hula chumvi ya jumba la mfalme* na si vema kwetu kuona masilahi ya mfalme yakiathiriwa, ndiyo sababu tumetuma barua ili kumjulisha mfalme jambo hilo, 15 ili uchunguzi ufanywe katika kitabu cha kumbukumbu za mababu zako.+ Ndipo utakapoona katika kitabu hicho cha kumbukumbu kwamba hili ni jiji lenye uasi, linalowaletea hasara wafalme na mikoa,* na tangu zamani lilikuwa na wachochezi wa uasi. Ndiyo sababu jiji hili liliangamizwa.+
-