-
Ezra 2:59-63Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
59 Na hawa ndio waliopanda kutoka Tel-mela, Tel-harsha, Kerubi, Adoni, na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kama ukoo wao* na asili yao ilikuwa ya Waisraeli:+ 60 wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, 652. 61 Na kutoka kwa wana wa makuhani: wana wa Habaya, wana wa Hakozi,+ wana wa Barzilai, aliyemwoa mmoja kati ya mabinti wa Barzilai+ Mgileadi na kuitwa kwa jina lao. 62 Hao walichunguza kumbukumbu zao ili wathibitishe ukoo wao, lakini hawakupata majina ya koo zao, kwa hiyo hawakustahili kuwa makuhani.*+ 63 Gavana* akawaambia kwamba hawangeweza kula vitu vitakatifu kabisa+ mpaka apatikane kuhani ambaye angechunguza Urimu na Thumimu.+
-