-
Mwanzo 22:10-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Kisha Abrahamu akaunyoosha mkono wake na kuchukua kisu* ili amuue mwanawe.+ 11 Lakini malaika wa Yehova akamwita kutoka mbinguni: “Abrahamu, Abrahamu!” naye akajibu: “Mimi hapa!” 12 Kisha akasema: “Usimdhuru mvulana huyo, wala usimtendee lolote, kwa maana sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu kwa sababu hukuninyima+ mwana wako, mwana wako wa pekee.”
-