-
Yeremia 12:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Wewe ni mwadilifu, Ee Yehova,+ ninapokuletea malalamishi yangu,
Ninapozungumza nawe kuhusu mambo ya haki.
Lakini kwa nini njia ya waovu imefanikiwa,+
Na kwa nini watu wenye hila hawana wasiwasi?
2 Uliwapanda, nao wametia mizizi.
Wamekua na kuzaa matunda.
Wewe uko kwenye midomo yao, lakini uko mbali na mawazo yao ya ndani kabisa.*+
3 Lakini unanijua vema, Ee Yehova,+ unaniona;
Umeuchunguza moyo wangu na kuupata ukiwa katika muungano nawe.+
Waweke kando kama kondoo wa kuchinjwa,
Na uwatenge kwa ajili ya siku ya kuuawa.
-