-
Kutoka 7:20, 21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Mara moja Musa na Haruni wakafanya kama Yehova alivyowaamuru. Akaiinua fimbo hiyo na kuyapiga maji ya Mto Nile mbele ya Farao na watumishi wake, na maji yote yaliyokuwa katika Mto Nile yakabadilika na kuwa damu.+ 21 Basi samaki waliokuwa mtoni wakafa,+ na mto ukaanza kunuka, na Wamisri hawakuweza kunywa maji ya Mto Nile,+ kulikuwa na damu katika nchi yote ya Misri.
-