-
1 Samweli 1:10, 11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Hana alikuwa na uchungu mwingi sana,* akaanza kusali kwa Yehova+ na kulia sana. 11 Naye akaweka nadhiri hii: “Ee Yehova wa majeshi, ikiwa utayaona mateso yangu mimi mtumishi wako na kunikumbuka na usiponisahau mimi mtumishi wako, nawe unipe mtoto wa kiume,+ nitamtoa awe wa Yehova sikuzote za maisha yake, na hakuna wembe utakaogusa kichwa chake.”+
-
-
2 Samweli 16:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Kisha Daudi akamwambia Abishai na watumishi wake wote: “Ikiwa mwanangu mwenyewe, niliyemzaa anatafuta uhai wangu,*+ je, Mbenjamini hatafanya zaidi?+ Mwacheni anitukane, kwa maana Yehova alimwambia afanye hivyo! 12 Huenda Yehova ataona mateso yangu,+ na Yehova atanilipa kwa wema badala ya matusi niliyotukanwa leo hii.”+
-