Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 14:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Sasa Musa akaunyoosha mkono wake juu ya bahari;+ naye Yehova akaisukuma bahari nyuma usiku kucha kwa upepo wenye nguvu wa mashariki, maji yakagawanyika,+ kukawa na nchi kavu+ katikati ya bahari.

  • Hesabu 11:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Kisha upepo kutoka kwa Yehova ukavuma ghafla na kuanza kuleta kware kutoka baharini na kuwaangusha kotekote kambini,+ kwenye eneo la umbali wa siku moja hivi kila upande kuzunguka kambi, wakafikia kimo cha mikono miwili* hivi kutoka ardhini.

  • Yeremia 10:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Anapofanya sauti yake isikike,

      Maji yaliyo mbinguni husukasuka,+

      Naye huyafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia.+

      Hutengeneza radi* kwa ajili ya mvua,

      Naye huutoa upepo katika maghala yake.+

  • Yeremia 51:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Anapofanya sauti yake isikike,

      Maji yaliyo mbinguni huwa na msukosuko,

      Naye huyafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia.

      Hutengeneza radi* kwa ajili ya mvua,

      Naye huutoa upepo katika maghala yake.+

  • Yona 1:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Ndipo Yehova akavumisha upepo mkali baharini, dhoruba* kali sana ikatokea baharini hivi kwamba meli ikawa karibu kuvunjika-vunjika.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki