16 Ni lazima Waisraeli washike Sabato; ni lazima waadhimishe Sabato katika vizazi vyao vyote. Ni agano la kudumu. 17 Ni ishara ya kudumu kati yangu na Waisraeli,+ kwa sababu katika siku sita mimi, Yehova, niliziumba mbingu na dunia na katika siku ya saba nilipumzika na kustarehe.’”+