-
Matendo 4:25-28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 nawe ulisema kupitia roho takatifu kwa kinywa cha babu yetu Daudi,+ mtumishi wako: ‘Kwa nini mataifa yalikuwa na msukosuko na watu wakatafakari mambo matupu? 26 Wafalme wa dunia walijipanga nao watawala wakakusanyika pamoja kama kitu kimoja dhidi ya Yehova* na dhidi ya mtiwa-mafuta wake.’*+ 27 Kwa kweli Herode na Pontio Pilato+ pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli walikusanyika katika jiji hili dhidi ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, ambaye ulimtia mafuta,+ 28 ili wafanye yale ambayo mkono na shauri lako liliazimia awali yatukie.+
-