15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi;
Wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.+
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri+
Wala kwa madini ya shohamu na yakuti yasiyopatikana kwa urahisi.
17 Dhahabu na kioo haviwezi kulinganishwa nayo;
Wala haiwezi kubadilishwa kwa chombo cha dhahabu bora.+
18 Marijani na fuwele hazistahili kutajwa,+
Kwa maana mfuko uliojaa hekima una thamani kuliko mfuko uliojaa lulu.