Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 8:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Akasema: “Mfalme atakayewatawala atakuwa na haki ya kudai mambo haya:+ Atawachukua wana wenu+ na kuwafanya wawe waendeshaji wa magari yake ya farasi+ na wapanda farasi wake,+ na baadhi yao watalazimika kukimbia mbele ya magari yake. 12 Naye atajichagulia wakuu wa maelfu+ na wakuu wa hamsini,+ na baadhi yao watamlimia mashamba yake,+ watavuna mazao yake,+ na kutengeneza silaha zake za vita na vifaa vya magari yake.+

  • 1 Wafalme 4:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Sulemani alikuwa na wasaidizi 12 waliowasimamia Waisraeli wote waliomwandalia chakula mfalme na nyumba yake. Kila mmoja wao alikuwa na jukumu la kuandaa chakula mwezi mmoja kwa mwaka.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 26:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Isitoshe, Uzia alijenga minara+ Yerusalemu karibu na Lango la Pembeni,+ Lango la Bondeni,+ na Nguzo ya Kutegemeza Ukuta, naye akaiimarisha. 10 Pia, alijenga minara+ nyikani na kuchimba* matangi mengi ya maji (kwa maana alikuwa na mifugo mingi sana); alifanya hivyo pia katika Shefela na katika nchi tambarare ya juu. Alikuwa na wakulima na watunzaji wa mizabibu milimani na kule Karmeli, kwa maana alipenda kilimo.

  • Wimbo wa Sulemani 8:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Sulemani alikuwa na shamba la mizabibu+ kule Baal-hamoni.

      Aliwakabidhi watunzaji shamba hilo la mizabibu.

      Kila mmoja wao alikuwa akileta vipande elfu moja vya fedha kwa ajili ya matunda yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki